Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mjumbe wa KM kwa Darfur kuhimiza makundi yote husika kushiriki katika mazungumzo ya amani ya Sirte

Mjumbe wa KM kwa Darfur kuhimiza makundi yote husika kushiriki katika mazungumzo ya amani ya Sirte

Mjumbe Maalumu wa KM kwa Darfur, Jan Eliasson alifanya mahojiano na waandishi habari waliopo Makao Makuu, kwa kutumia njia ya vidio, kutokea Asmara, Eritrea ambapo alidhihirisha ya kuwa hana uhakika juu ya viongozi wa makundi ya waasi na wapinzani wepi watakaoshiriki kwenye mazungumzo ya upatanishi yanayofanyika mwisho wa wiki kwenye mji wa Sirte, Libya.