Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mawaziri wanazingatia msukumo mpya kugharamia maendeleo

Mawaziri wanazingatia msukumo mpya kugharamia maendeleo

Mkutano wa Hadhi ya Juu ulifanyika kwenye Makao Makuu mjini New York kusailia hatua za kuchukuliwa kukamilisha maafikiano yaliopitishwa mwaka 2000 kwenye mji wa Monterrey, Mexico. Maafikiano ya Monterrey hasa yalidhamiria kuongeza ushirikiano wa kiuchumi wenye nguvu, na ulio bora, kwa umma wa kimataifa ili kupiga vita umasikini. Maafikiano ya Monterrey yalipendekeza kuzingatiwe masuala yanayoambatana na usimamizi wa kizalendo wa gharama za kuhudumia maendeleo; na kusailia taratibu madhubuti za ugawaji wa misaada ya kimataifa. ~~Sikiliza ripoti kamili kwenye idhaa ya mtandao.