Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ofisa wa UM ashiriki kwenye mjadala wa amani ya Cote d'Ivoire

Ofisa wa UM ashiriki kwenye mjadala wa amani ya Cote d'Ivoire

Abou Moussa, Ofisa anayeshughulikia Opereseheni za Amani za UM katika Cote d’Ivoire alikuwa miongoni mwa wajumbe walioshiriki kwenye duru mpya ya mazungumzo ya kuhakikisha mafanikio katika kutekeleza maafikiano ya kisiasa yaliofikiwa mapema mwaka huu miongoni mwa viongozi wa taifa liliogawanyika la Afrika Magharibi. Mazungumzo haya ya amani yalifanyika mwanzo wa wiki kwenye mji wa Ouagadougou, Burkina Faso na kulitathiminiwa namna ya kutekeleza, kwa ridhaa ya wote, maafikiano yanayohusu usalama wa Waziri Mkuu, kuthibitisha vyeo vya maofisa wa kundi la waasi la Forces Nouvelles na pia hatua za kuchukuliwa juu ya usalama wa makamishna wa mikoa baada ya kuenezwa katika sehemu mbalimbali za nchi.