Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mtaalamu wa UM juu ya Haki za Watoto anazuru Cote d'Ivoire

Mtaalamu wa UM juu ya Haki za Watoto anazuru Cote d'Ivoire

Radhika Coomaraswamy, Mjumbe Maalumu wa UM anayehusika na Haki za Watoto kwenye Mazingira ya Vita, wiki hii ameanza ziara rasmi katika Cote d’Ivore, baada ya kuitika mwaliko wa Serekali ya taifa hilo. Coomaraswamy alitarajiwa kuendeleza ukaguzi juu ya utekelezaji wa miradi ya kuwarudisha, kwa jamii zao, wale watoto walioshiriki kwenye mapigano. Kadhalika Coomaraswamy anatazamiwa kusailia vitendo karaha cha kutumia mabavu kuwaingilia baada ya vita kumalizika.