Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

WFP inaomba dola milioni 80 kusaidia chakula wahamiaji Chad

WFP inaomba dola milioni 80 kusaidia chakula wahamiaji Chad

Shirika la UM juu ya Miradi ya Chakula Duniani (WFP) limetoa mwito wa dharura, wiki hii, wenye kuitaka jumuiya ya kimataifa kuchangisha dola milioni 80 kusaidia chakula wahamiaji na wahajiri wa ndani ya nchi 400,000 waliopo Chad mashariki. WFP ilisema mchango huu unahitajika mwezi ujao, ili kuhakikisha kutakuwepo chakula cha kutosha kwa umma muhitaji kabla ya majira ya mvua kuwasili.