Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mazungumzo na Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Asha-Rose Migiro

Mazungumzo na Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Asha-Rose Migiro

Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Asha-Rose Migiro alifanya mazungumzo maalumu na Idhaa ya Kiswahili ya Redio ya UM ambapo alichukua fursa hiyo kufafanua mwelekeo mpya kuhusu kazi na shughuli za UM duniani. Alisailia juu ya juhudi za KM Ban Ki-moon katika kuharakisha utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo ya Milenia (MDGs), kwa wakati, Afrika kusini ya Sahara. Kwenye makala hii ya awali ya mahojiano yetu Naibu KM Migiro anazugumzia mada mbili: awali, utekelezaji wa Malengo ya MDGs Afrika kusini ya Sahara na, pili, suala la Darfur. ~~Sikiliza ripoti kamili kwenye idhaa ya mtandao.