Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mjumbe wa UM kwa tatizo la Uganda kaskazini afanyisha mazungumzo ya amani na viongozi husika

Mjumbe wa UM kwa tatizo la Uganda kaskazini afanyisha mazungumzo ya amani na viongozi husika

Wiki hii Raisi mstaafu wa Msumbiji, Joaquim Chissano na pia Mjumbe Maalumu wa KM juu ya mzozo wa sugu wa Uganda kaskazini, ameanza kukutana kwa mazungumzo ya amani na viongozi kadha wa eneo, ikiwa miongoni mwa juhudi za kimataifa za kuwasilisha suluhu ya kudumu kati ya makundi yanayohasimiana, yaani Serekali ya Uganda na kundi la waasi la LRA.