Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNHCR yajaribu kutafuta suluhu ya muda mrefu kwa raia wa Eritrea

UNHCR yajaribu kutafuta suluhu ya muda mrefu kwa raia wa Eritrea

Shirika la UM juu ya Wahamiaji (UNHCR) limeripoti kuwa hivi sasa linashiriki kwenye jitihadi za kimataifa za kutafuta suluhu ya muda mrefu kwa raia wa Eritrea 130,000 waliokwama katika kambi 12 za wahamiaji ziliopo Sudan mashariki.