Skip to main content

Waathiriwa wa mafuriko milioni 1.5 katika Sudan kufadhiliwa dola milioni 8.7 na UM

Waathiriwa wa mafuriko milioni 1.5 katika Sudan kufadhiliwa dola milioni 8.7 na UM

Waathiriwa milioni 1.5 (moja na nusu) wa mafuriko yaliotukia karibuni Sudan watafadhiliwa msaada wa dola milioni 8.7 kutoka ule Mfuko Maalumu wa Misaada ya Dharura wa UM, yaani Mfuko wa CERF. Fedha hizi zitatumiwa kupeleka misaada ya kiutu na kukidhia mahitaji ya dharura ya umma husika nchini Sudan.