Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mzozo wa mgomo wa watumishi wazalendo wa MONUC katika DRC

Mzozo wa mgomo wa watumishi wazalendo wa MONUC katika DRC

Jumuiya ya Watumishi Wazalendo walioajiriwa na Shirika la UM linalosimamia ulinzi wa amani katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, yaani Shirika la MONUC, Alkhamisi iliamua kuitisha mgomo baridi, uliosababishwa na madai ya kwamba wenye kusimamia utawala katika MONUC walipuuza kwa muda mrefu malalamiko yao ya kikazi na kushindwa kuwapatia suluihu ya kuridhisha. Tulifanya mahojiano ya simu na mwandishi habari aliopo mjini Kinshasa, DRC anayeitwa ‘Ahmed Simba’ ambaye alitupatia dokezo kuhusu mgomo huu. Alianza kwa kuelezea nini hasa kilikuwa chanzo cha mgomo.~~Sikiliza mahojiano kamili kwenye idhaa ya mtandao.