Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Raia wa Uchina kuongoza vikosi vya amani vya UM

Raia wa Uchina kuongoza vikosi vya amani vya UM

Meja-Jenerali Zhao Jingmin wa Jamhuri ya Umma wa Uchina ameteuliwa na KM Ban Ki-moon kuwa Kamanda Mkuu mpya wa vikosi vya ulinzi wa amani vya UM katika Sahara ya Magharibi (MINURSO). Hii itakuwa ni mara ya kwanza kwa raia wa Uchina kuongoza operesheni za ulinzi wa amani za UM duniani.