Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mazungumzo ya upatanishi ya Mogadishu kupongezwa na Mjumbe wa KM kwa Usomali

Mazungumzo ya upatanishi ya Mogadishu kupongezwa na Mjumbe wa KM kwa Usomali

Francois Lonseny Fall, Mjumbe Maalumu wa KM kwa Usomali akiongoza ujumbe wa Kamati ya Ushauri ya Kimataifa Alkhamisi walihudhuria mjini Mogadishu taadhima za kufunga Mkutano wa Upatanishi wa Taifa. Fall aliwapongeza wawakilishi wote walioshiriki kwenye mkutano ambao alisema ulimalizika kwa mafanikio ya kutia moyo, kwa sababu ya mchango wa serekali umma wa Usomali ambao pamoja waliamua kuwasilisha suluhu ya kizalendo.