Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNHCR na IMO yatoa mwito kupunguza vifo baharini

UNHCR na IMO yatoa mwito kupunguza vifo baharini

Shirika la wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR na shirika la kimataifa la safari za baharini IMO, yameungana kutoa mwito wa kuchukuliwa hatua zaidi kuzuia vifo vinavyo tokea miongoni mwa watu wanaosafiri kwa maboti katika safari za hatari kabisa kuvuka bahari ya Mediterranean, Ghuba ya aden na kwengineko kujaribu kutafuta maisha bora.