Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UM walaani vikali ukatili na mauaji karaha yaliotukia DRC Mashariki

UM walaani vikali ukatili na mauaji karaha yaliotukia DRC Mashariki

Shirika la UM juu ya Ulinzi wa Amani katika JKK (MONUC) limeripoti kutukia karibuni katika vijiji vya Nyabuluze na Mhungu, Kivu ya Kusini mashambulio yasiochokozwa, ambapo raia 19 waliuawa, wakiwemo watoto wadogo na wanawake. Wanamgambo wa Rasta pamoja na waasi wa kundi la Rwanda linaloitwa FDLR ndio wanaotuhumiwa kuendeleza vitendo hivi vilivyoharamisha mipaka ya kiutu.