Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kesi ya Charles Taylor kuanzishwa mjini Hague

Kesi ya Charles Taylor kuanzishwa mjini Hague

KM Ban amepongeza kuanzishwa kwa kesi ya aliyekuwa Raisi wa Liberia, Charles Taylor katika mji wa Hague, Uholanzi na Mahakama Maalumu ya Sierra Leone dhidi ya Jinai ya Vita. Taylor alituhumiwa kuongoza vitendo karaha viliokiuka sheria na kupalilia uhasama miongoni mwa vikundi vya kizalendo vilivyokuwa vimeshiriki kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe katika Sierra Leone.