Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ukame wazusha upungufu mkubwa wa chakula Lesotho

Ukame wazusha upungufu mkubwa wa chakula Lesotho

Ripoti mpya ya Shirika la UM juu ya Chakula na Kilimo (FAO) pamoja na Shirika la Miradi ya Chakula Duniani (WFP) imedhihirisha ya kwamba khumsi moja ya idadi ya watu nchini Lesotho, yaani watu 400,000, inakabiliwa na tatizo hatari la ukosefu mkubwa wa chakula, kufuatia ukame mbaya uliotanda karibuni kwentye taifa hilila kusini ya Afrika. Kwa mujibu wa taarifa UM hali hii haijwahai kuhushudiwa kieneo kwa muda wa miaka 30 ziada. Jumuiya ya kimataifa pamoja na wahisani wa kimataifa, wamehimizwa kushirikiana kipamoja kupeleka misaada ya dharura ya kihali, na pia misaada ya chakula, kwa Lesootho na katika mataifa jirani yanayokabiliwa na tatizo la ukame mbaya ili kunusuru maisha ya mamilioni ya raia wa kusini ya Afrika.