Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Baraza la Usalama lataka kuanzishwe tume ya kuchunguza vikwazo dhidi ya Charles Taylor

Baraza la Usalama lataka kuanzishwe tume ya kuchunguza vikwazo dhidi ya Charles Taylor

Baraza la Usalama limepitisha kwa kauli moja azimio linalomtaka KM Ban Ki-moon kuanzisha tume maalumu ya wataalamu wa shughuli za fedha na biashara ya almasi, watakaopewa madaraka ya kuchunguza “madai yanayoaminika” dhidi ya Raisi wa zamani wa Liberia Charles Taylor, madai yenye kusisitiza kuwa Taylor bado ana uwezo na fursa ya kutumia kuhodhi mali nyingi sana ambayo imeekewa vikwazo na Baraza la Usalama mwaka 2004, licha ya kuwa Taylor sasa hivi yumo kizuizini.