Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

NKM atahudhuria Mkutano Mkuu wa AU Ghana

NKM atahudhuria Mkutano Mkuu wa AU Ghana

Naibu KM (NKM) Asha-Rose Migiro anatazamiwa kuelekea Afrika na Ulaya mwisho wa wiki. NKM atamwakilisha KM kwenye Mkutano Mkuu wa Umoja wa Afrika (AU) utakaofanyika mwanzo wa Julai mjini Accra, Ghana. Kabla ya hapo NKM Migiro ataelekea Vienna, Austria kutoa hutuba ya ufunguzi kwenye \'Jopo la 7 la Dunia la Uvumbuzi Mpya Ziada wa Shughuli za Serikali\'. Baada ya hapo ataelekea Guinea-Bissau, ikiwa ziara ya kwanza rasmi ya KM au NKM tangu taifa hilo kujiunga na UM.