Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Watuhumiwa watatu wa makosa ya vita Sierra Leone kupatikana na hatia ya mashtaka 11

Watuhumiwa watatu wa makosa ya vita Sierra Leone kupatikana na hatia ya mashtaka 11

Mahakama Maalumu juu ya Jinai ya Vita Sierra Leone imetoa hukumu yake ya kwanza wiki hii ambapo watuhumiwa watatu wa Jeshi la Baraza la Mapinduzi – yaani Alex Tamba Brima, Brima Bazzy Kamara na Santigie Borbor Kanu - walipatikana na hatia ya mashtaka 11 yanayohusikana na makosa ya vita na vile vile jinai dhidi ya utu. Hukumu juu ya adhabu ya watuhumiwa hawa itatolewa na Mahakama kati ya mwezi Julai.