Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Hali ya uchumi na jamii duniani kwa 2007

Hali ya uchumi na jamii duniani kwa 2007

Ripoti ya UM juu ya Uchunguzi wa Hali ya Uchumi na Jamii Duniani kwa 2007 ilioelezewa kwa muktadha usemao \'Maendeleo katika Dunia yenye Kuzeeka\' iliwakilishwa wiki hii mbele ya waandishi habari wa kimataifa na Jose Antonio Ocampo, Makamu KM anayehusika na masuala ya uchumi na jamii. Ripoti iliashiria ya kuwa watu milioni 1.2 wenye umri wa miaka 60 na zaidi, watakuwa wanaishi kwenye mazingira ya hali iliokosa kile kinachojulikana kama ‘wavu wa hifadhi ya jamii’. Asilimia 80 ya fungu hili la umma wa kimataifa litakutikana zaidi katika mataifa yanayoendelea.

Sikiliza ripoti kamili kwenye idhaa ya mtandao.