Kikao maalumu Libya kusailia mzozo wa Darfur
Jan Eliasson, Mjumbe Maalumu wa KM kwa Darfur alihudhuria kikao maalumu kilichoandaliwa na Libya majuzi kuzingatia hali katika Darfur. Kwenye kikao hicho walijumuika wawakilishi kutoka Sudan, Chad, Misri, Eritrea na pia Libya, Uchina, Ufaransa, Uingereza, Marekani, Kanada, Uholanzi, Norway na pamoja na wajumbe waliowakilisha Umoja wa Afrika (AU), Umoja wa Ulaya (EU) na Umoja wa Nchi Huru za Kiarabu. Wawakilishi wote hawa waliafikiana juu ya ulazima wa kuharakisha suluhu ya jumla, na ya kudumu, kuhusu vurugu la Darfur.