Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

ICC yatoa hatia ya kukamata watuhumiwa wa jinai ya Darfur

ICC yatoa hatia ya kukamata watuhumiwa wa jinai ya Darfur

Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ya Halaiki (ICC) imetoa hati ya kuwakamata Ahmed Muhammad Haroun, Waziri wa Masuala ya Kiutu katika Sudan na vile vile kiongozi wa wanamgambo wa Janjaweed, Ali Muhammad Al Abd-Al-Rahman baada ya kutuhumiwa na Mahakama kuwa wanahusikana na jinai ya vita na kushiriki kwenye vitendo vilivyokiuka utu katika eneo la Darfur.