Hali Usomali inaendelea kuharibika
Wataalamu 12 wa UM wametangaza, hadharani, taarifa ya pamoja iliodhirisha wasiwasi wao mkubwa juu ya athari za uhasama uliofumka karibuni kwenye mji wa Mogadishu, Usomali, ambapo mamia ya watu waliuawa na mamia elfu ya raia kulazimika kuhajiri makazi.