Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mkataba wa Haki za Watu Walemavu Duniani

Mkataba wa Haki za Watu Walemavu Duniani

Katika makala iliopita, iliwakilisha sehemu ya kwanza ya mazungumzo kati ya Redio ya UM na Maalim Khalfan Hemed Khalfan, Mkurugenzi Mtendaji wa Umoja wa Watu Walemavu Zanzibar (UWZ)ambapo alielezea juu ya mataifa 80 ziada yalioridhia kutia sahihi Mkataba mpya wa Haki za Walemavu Duniani, yakijumuisha mataifa ya Afrika Mashariki ya Kenya, Tanzania na Uganda. Kadhalika, Maalim Khalfan alielezea umuhimu wa kuwepo ushirikianao wa kipamoja kati ya mataifa kwenye utekelezaji wa mapendekezo ya Mkataba huo, kwa sababu, alikumbusha, sio Mataifa yote Wanachama yenye uwezo au nyenzo za kuzitekeleza haki za kimsingi za watu walemavu. Halkadhalika, alitupatia dokezo juu ya tafsiri ya mtu mlemavu, kama inavyotafsiriwa na Mkataba, na alifahamisha fungamano ziliopo za kisheria zinazoyawajibisha mataifa yaliouridhia na kuuidhinisha Mkataba kuwatekelezea watu wenye ulemavu haki zao.

Sikiliza mahojiano kamili kwenye idhaa ya mtandao.