Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mahakama Maalumu ya Sierra Leone imetangaza tarehe ya kesi ya C. Taylor

Mahakama Maalumu ya Sierra Leone imetangaza tarehe ya kesi ya C. Taylor

Mahakama Maalumu kwa Sierra Leone inayohusika na kesi za jinai ya vita imetangaza rasmi kuwa utaanza kusikiliza kesi ya aliyekuwa Raisi wa Liberia, Charles Taylor mnamo tarehe 04 Juni mwaka huu. Uamuzi huu ulifikiwa kwenye kikao kilichokutana kwenye mji wa Hague, Uholanzi kuandaa taratibu za usikilizaji wa mashtaka. Taylor ametuhumiwa makosa 11 yanayoambatana na makosa ya kushiriki kwenye jinai ya vita pamoja na ukiukaji uliovuka mipaka ya sheria ya kimataifa dhidi ya utu, ikijumuisha mauaji ya halaiki, vitendio vya kunajisi kihorera, ukataji viungo, utumwa wa kijinsia na kuwalazimisha watoto wenye umri mdogo kupigana.