Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Vikosi vya MONUC katika DRC vinachunguzwa kuhusu rushwa

Vikosi vya MONUC katika DRC vinachunguzwa kuhusu rushwa

Ofisi ya UM ya Kuchunguza Ukiukaji Kanuni za Kazi (OIOS) imeripotiwa kuendeleza ukaguzi wa hali ya juu kuhusu yale madai kwamba vikosi vya ulinzi wa amani vya UM katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo vya Shirika la MONUC, vilihusika na biashara ya magendo ya madini katika kipindi kati ya miaka ya 2005-2006. Tuhuma zilidai vikosi vya MONUC vilinunua madini ya thamani kwa kuwapatia wachuuzi madini hayo silaha, biashara inayodaiwa kuendelezwa kwenye mji wa Mongwalu, Wilaya ya Ituri iliopo Mashariki ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC).