Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

ICTR imeidhinisha hukumu ya kifungo cha maisha dhidi ya M. Muhimana

ICTR imeidhinisha hukumu ya kifungo cha maisha dhidi ya M. Muhimana

Korti Ndogo ya Rufaa ya Mahakama ya Kimataifa juu ya Rwanda (ICTR) iliopo Arusha, Tanzania imeidhinisha na kuthibitisha tena ile hukumu ya 2005 ya kifungo cha maisha kwa Mikaeli Muhimana aliyetuhumiwa kuendeleza makosa ya jinai dhidi ya utu katika Rwanda mnamo 1994. Miongoni mwa makosa yaliyomtia hatiani Muhimana ni pamoja na kushtakiwa kushiriki kwenye jinai ya mauaji ya halaiki, vitendo vya kunajisi kihorera wanawake wawili na vile vile kumwua mwanamke mwengine mja mzito.