Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Fafanuzi za kikao cha 51 cha Kamisheni ya CSW kuhusu haki za wanawake

Fafanuzi za kikao cha 51 cha Kamisheni ya CSW kuhusu haki za wanawake

Kamisheni ya Baraza Kuu la UM juu ya Hadhi na Haki za Wanawake, au Kamisheni ya CSW, karibuni ilikutana kwenye Makao Makuu ya UM mjini New York, na kuzingatia utaratibu wa kuchukuliwa na nchi wanachama kuharakisha utekelezaji wa ile mikataba na miradi iliopitishwa na kuidhinishwa kimataifa, inayohusu haki za wanawake, ili kulipatia fungu hili la kijinsia ulinzi halali dhidi ya vitendo vya kibaguzi.~

Rachel B. Dzombo, Katibu wa Kudumu wa Wizara ya Jinsia, Riadha, Utamaduni na Huduma za Jamii katika Kenya alikuwa miongoni mwa wajumbe kutoka Afrika Mashariki waliohudhuria kikao cha 51 cha Kamisheni ya CSW, na alikubaliana na uchambuzi wa Naibu KM juu ya hadhi ya wanawake ulimwenguni na mzoroto uliopo ulimwenguni katika kuwatekelezea haki zao kama inavyostahiki. Kwenye mazungumzo niliyoyafanya kwenye studio zetu Bi Dzombo, anatufafanulia zaidi maoni yake kuhusu namna mijadala ya Kamisheni ya CSW ilivyoendeshwa, na pia kusailia harakati za kimataifa zinazohitajika kuwatekelezea wanawake na watoto wa kike haki halali za kimsingi.

Sikiliza idhaa ya mtandao kwa mahojiano kamili.