UM unahimiza upatanishi na amani irudishwe Usomali
Mjumbe Maalumu wa KM kwa Usomali, Francois Lonseny Fall wiki hii alihudhuria Mkutano wa Amani wa Pande Tatu kwa Usomali uliofanyika Cairo, Misri na kusimamiwa Shirika la Mawasiliano ya Kimataifa kwa Somalia (IGAD). Alipowasilisha risala yake mkutanoni Fall alionya dhidi ya kitendo cha kupokonya silaha kwa nguvu makundi yanayohasimiana mjini Mogadishu, ikiwa lengo la operesheni hizo ni kuwasilisha mazingira yatakayoruhusu mkutano wa upatanishi kufanyika kwenye mji mkuu huo.