Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ajenda ya BU kwa Aprili itaongozwa na masuala ya Darfur na mabadiliko ya hali ya hewa

Ajenda ya BU kwa Aprili itaongozwa na masuala ya Darfur na mabadiliko ya hali ya hewa

Balozi Emyr Jones Parry wa Uingereza aliwaambia wanahabari wa kimataifa kwenye Makao Makuu mjini New York, ya kwamba kutokana na muongezeko wa vurugu na hali ya wasiwasi katika jimbo la uhasama la Darfur, Sudan na athari zake kwa mataifa jirani, na pia tatizo la madhara ya mabadiliko ya hali ya hewa ulimwenguni, Baraza la Usalama limeamua kuyapa masuala haya umuhimu zaidi katika mijadala yake ya Aprili.

Uingereza ni mwenyekiti wa Baraza la Usalama kwa mwezi Aprili.