Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Tume ya wataalamu wa UM kwenda Bukini kuratibu mradi wa kuwasaidia waathiriwa wa vimbunga

Tume ya wataalamu wa UM kwenda Bukini kuratibu mradi wa kuwasaidia waathiriwa wa vimbunga

Ofisi ya UM juu ya Misaada ya Dharura (OCHA) imetuma Bukini timu maalumu ya wataalamu watano watakaofanya uchunguzi wa mahitaji ya kihali katika eneo hilo, na pia kuandaa utaratibu wa kuhudumia misaada ya kimataifa kwa umma ulioathirika na maafa ya vimbunga, maafa asilia ambayo yalileta uharibifu mkubwa kwenye taifa hilo la kisiwa.