Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Meli iliokodiwa na WFP na kutekwa nyara Usomali imeachiwa huru

Meli iliokodiwa na WFP na kutekwa nyara Usomali imeachiwa huru

Shirika la UM juu ya Miradi ya Chakula Duniani (WFP) limepongeza kuachiwa huru kwa ile meli ya MV Rozen, ambayo iliikodi siku za nyuma kupeleka chakula Usomali. Meli hiyo ilitekwa nyara na maharamia kwenye mwambao wa eneo la Puntland mnamo Februari 25 mwaka huu.