Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Matatizo ya kiutu kukithiri katika CAR

Matatizo ya kiutu kukithiri katika CAR

Shirika la Miradi ya Chakula Duniani (WFP) limeripoti kwamba hali mbaya ya kiutu inaendelea kusambaa katika Jamhuri ya Afrika ya Kati (CAR) ambapo mamia elfu ya raia waliong’olewa makwao, kwa sababu ya hali ya vita na mapigano ya wenyewe kwa wenyewe, wanahitajia kufadhiliwa kidharura misaada ya chakula kunusuru maisha. Hali hii sasa hivi imechafuliwa zaidi kutokana na vurugu liliofumka na kufurika kutokea eneo jirani la Darfur, Sudan.