Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mkataba wa Haki za Watu Walemavu Duniani Kuridhiwa Kimataifa (Sehemu ya Kwanza)

Mkataba wa Haki za Watu Walemavu Duniani Kuridhiwa Kimataifa (Sehemu ya Kwanza)

Mnamo mwisho wa mwezi Machi, Mataifa Wanachama 81 pamoja na Umoja wa Ulaya (EU) walijumuika kwenye Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa (UM) kutia sahihi mkataba mpya wa kihistoria, uliokusudiwa kuboresha maisha ya watu milioni 650 walemavu duniani na kuwatekelezea haki zao za kimsingi kama inavyostahiki. Mkataba huu, kwa ujumla, unakataza na kupiga marufuku, ubaguzi wa aina yoyote, katika sehemu zote za jamii dhidi ya watu walemavu.

Sikiliza taarifa kamili kwenye idhaa ya mtandao.