Naibu KM azuru DRC kuimarisha amani
Naibu KM Asha-Rose Migiro wiki hii alifanya ziara ya siku tatu katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC). Alipokuwepo huko alikutana kwa mazungumzo, na pia mashauriano, na Raisi Joseph Kabila pamoja na viongozi kadha wengine wa kisiasa, wakijumuisha vile vile wanasiasa wa kutoka vyama vya upinzani.