Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

KM kuhimiza suluhu ya amani kwa Darfur

KM kuhimiza suluhu ya amani kwa Darfur

KM Ban Ki-moon amemtumia Raisi Omar Hassan Al Bashir wa Sudan, kwa mara nyengine tena barua yenye kuelezea, kwa ukamilifu, utaratibu na hatua za kuchukuliwa zitakazorahisisha ile rai ya kupeleka vikosi vya mseto vya ulinzi wa amani vya UM na AU katika Darfur, majeshi ambayo idadi yao inakadiriwa kufikia askari 24,000.