Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

WFP imewaomba maharamia kuachia huru mabaharia wa meli yake

WFP imewaomba maharamia kuachia huru mabaharia wa meli yake

Shirika la UM juu ya Miradi ya Chakula Duniani (WFP) limewaomba wale maharamia walioteka nyara karibuni ile meli iliokodiwa kupeleka chakula Usomali, wawaachie huru mabaharia na chombo chao ili waweze kuendelea kuhudumia kihali ule umma muhitaji wa eneo hilo la Pembe ya Afrika. Meli ya WFP iliyotekwa nyara imeripotiwa kutia nanga katika eneo liliopo karibu na Puntland, Usomali.~