Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Eritrea imemfukuza nchi mtaalamu wa UM juu ya mabomu ya kutegwa

Eritrea imemfukuza nchi mtaalamu wa UM juu ya mabomu ya kutegwa

Serekali ya Eritrea imeiarifu UM kumpiga marufuku nchini, Meneja wa Mradi wa UM unaosimamia Ufyekaji wa Mabomu Yaliotegwa Ardhini, David Bax kwa madai kuwa alikiuka sheria na kanuni za nchi. Shirika la UM linalosimamia uangalizi wa Eneo la Amani Mipakani kati ya Ethiopia na Eritrea (UNMEE) limeripoti kutokubaliana na madai hayo ya Serekali ya Eritrea. Hata hivyo, kwa mujibu wa ripoti za UNMEE, Bax ameshaondoka Eritrea kwa hivi sasa.~