Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Baraza la Usalama linazingatia masuala ya amani katika Afrika

Baraza la Usalama linazingatia masuala ya amani katika Afrika

Baraza la Usalama lilikutana kwenye kikao maalumu wiki hii kuzingatia ushirikiano kati ya mashirika ya kikanda na UM, hususan Umoja wa Nchi Huru za Afrika (AU) kwa makusudio ya kuimarisha usalama na amani. Kikao kilitilia mkazo umuhimu wa kukuza ushirikiano huo na kuboresha uhusiano mwema kati ya UM na AU, kwa matarajio ya kuzuia ugomvi na mapigano yanayozuka mara kwa mara barani Afrika, na kusimamia kipamoja taratibu zinazotakikana kuleta suluhu ya kudumu ya migogoro husika.