Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wapatanishi wa Darfur waonana na makundi ya Waarabu na wawakilishi wa jumuiya za kiraia

Wapatanishi wa Darfur waonana na makundi ya Waarabu na wawakilishi wa jumuiya za kiraia

Mjumbe wa KM kwa UM kwa Darfur, Balozi Jan Eliasson wa Usweden akifuatana na Dktr Salim Ahmed Salim, Mpatanishi wa Umoja wa Nchi Huru za Afrika (AU)kuhusu Darfur, wiki hii walikutana kwa mazungumzo mjini Khartoum na wawakilishi wa makundi ya makabila ya KiArabu, pamoja na viongozi wanaowakilisha jumuiya za kiraia, na kusailiana juu ya uwezekano wa kufufua tena mpango wa amani wa Darfur, kwa lengo la kukomesha haraka umwagaji wa damu kati ya makundi yanayohasimiana kwenye eneo hilo.