Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Watoto masikini na mayatima Zimbabwe kufadhiliwa misaada ya maendeleo na UM

Watoto masikini na mayatima Zimbabwe kufadhiliwa misaada ya maendeleo na UM

Shirika la UM juu ya Mfuko wa Maendeleo kwa Watoto (UNICEF) wiki hii limetiliana sahihi na Serekali ya Zimbabwe, pamoja na mashirika 21 yasio ya kiserekali, maafikiano ya kufadhilia jumuiya za kiraia misaada ya kuhudumia uandikishaji ziada wa watoto masikini na mayatima 350,000, ili waweze kuhudhuria masomo ya skuli za msingi. Vile vile msaada huo unatazamiwa kuwahudumia afya na kuboresha lishe watoto husika.