Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makundi husika na mzozo wa Darfur yakiri vurugu halizalishi suluhu, wabainisha Wapatanishi wa UM na AU

Makundi husika na mzozo wa Darfur yakiri vurugu halizalishi suluhu, wabainisha Wapatanishi wa UM na AU

Jan Eliasson, Mjumbe Maalumu wa KM kwa Darfur pamoja na Salim Ahmed Salim, Mpatanishi wa Darfur wa Umoja wa Nchi Huru za Afrika (AU) walikutana wiki hii nchini Sudan kwa mashauriano ya amani na viongozi wa wahamiaji wa ndani ya nchi, majemadari wa makundi ya waasi wasiotia sahihi Itifaki ya Amani ya Darfur, pamoja na machifu wa makabila kadhaa na vile vile wawakililishi wa Sereklali.