Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mtaalamu wa haki za kibinadamu kwa Usomali kuitaka serekali kuachia huru waandishi watatu wa habari

Mtaalamu wa haki za kibinadamu kwa Usomali kuitaka serekali kuachia huru waandishi watatu wa habari

Ghanim Alnajjar, Mtaalamu anayehusika na Haki za Kibinadamu katika Usomali amependekeza na kuawahimiza wenye madaraka Usomali kuwaachia huru, halan, wale waandishi habari watatu wa Kisomali walioshikwa karibuni na kuwekwa kizuizini. Alisema kitendo hiki kinatia wasiwasi na alikumbusha ya kwamba ni muhimu kwa vyombo vya habari kuwa na uwezo wa kueneza ripoti zao bila kuhofu wenye madaraka, msimamo ambao ukitekelezwa kama unavyotakikana ni kadhia itakayosaidia pakubwa kurfufua uslama na amani katika Usomali.