Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

WFP kununua chakula Msumbiji kuhudumia waathiriwa wa mafuriko

WFP kununua chakula Msumbiji kuhudumia waathiriwa wa mafuriko

Shirika la UM juu ya Miradi ya Chakula Duniani (WFP) limetoa mwito wa kufadhiliwa, kidharura, msaada wa fedha zinazohitajika kununua chakula kutoka Msumbiji, taifa liliodhurika na mafuriko kusini ya Afrika. Lengo la hatua hii ni kunusuru maisha ya raia muhitaji 120,000 walioathiriwa na mafuriko yalizka hivi karibuni katika taifa hilo.