Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

MONUC imethibitisha askari watoto wanaendelea kuajiriwa DRC, kinyume na kanuni za kimataifa

MONUC imethibitisha askari watoto wanaendelea kuajiriwa DRC, kinyume na kanuni za kimataifa

Shirika la UM juu ya Ulinzi wa Amani katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (MONUC)limethibitisha kwenye ripoti yake iliobainishwa wiki hii, ya kuwa askari watoto, wenye umri mdogo, bado wanaendelea kushinikizwa kusema uongo kuhusu umri wao na hadhi yao ya kiraia, ili wapate fursa ya kujiandikisha na jeshi jipya la muungano la taifa. TRukio hili limeshuhudiwa kujiri katika jimbo la Kivu Kaskazini.