Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mazungumzo ya amani kwa Darfur yafanyika Khartoum

Mazungumzo ya amani kwa Darfur yafanyika Khartoum

Shirika la UM juu ya Ulinzi wa Amani kwa Sudan (UNMIS) limeripoti kuwa Alkhamisi kulifanyika mkutano wa sita wa Utaratibu wa Amani wa Sehemu Tatu, katika mji wa Khartoum, Sudan ambapo kulijumuika wawakilishi wa Vikosi vya Ulinzi wa Amani vya Umoja wa Nchi Huru za Afrika (AU), wawakilishi wa UM pamoja na wale wa Serekali ya Sudan ambao walizingatia, kipamoja, furushi la mapendekezo ya kuimarisha zaidi operesheni za amani za vikosi vya AU katika Darfur.