Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mtumishi wa WFP kuuawa baada ya mashambulio ya kuvizia Sudan ya kusini

Mtumishi wa WFP kuuawa baada ya mashambulio ya kuvizia Sudan ya kusini

Emmanuel Chaku Joseph, mwenye umri wa miaka 28, raia wa Sudan aliyeajiriwa udereva na Shirika la UM juu ya Miradi ya Chakula Duniani (WFP) aliuawa kikatili mnamo kati ya wiki baada ya kuzingiwa na kushambuliwa kwenye barabara kati ya Juba, mji mkuu wa Sudan kusini na mji wa Torit.