Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UM waashiria mwelekeo wa uchumi wa dunia kwa 2007

UM waashiria mwelekeo wa uchumi wa dunia kwa 2007

Katika kila mwanzo wa mwaka, UM huwasilisha ripoti maalumu kuhusu mwelekeo wa maendeleo ya uchumi duniani, ripoti ambayo huandaliwa na idara mbalimbali za UM, ikijumuisha Idara Inayohusika na Masuala ya Kiuchumi na Jamii (DESA), Shirika la UM kuhusu Maendeleo ya Uchumi na Biashara (UNCTAD) pamoja na kamisheni tano za kikanda zinazoshughulikia huduma za uchumi, yaani Kamisheni ya ECA, kwa Afrika, ECE, kwa Mataifa ya Ulaya, ECLAC, kwa Amerika ya Latina na Maeneo ya Karibiani, ESCAP, kwa mataifa ya Asia na Pasifiki na vile vile Kamisheni ya ESCWA, inayohusika na maendeleo ya Asia ya Magharibi. ~~

Sikiliza taarifa kamili kwenye idhaa ya mtandao.