Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Didier Drogba ameteuliwa kuwa balozi mfadhili wa UNDP

Didier Drogba ameteuliwa kuwa balozi mfadhili wa UNDP

Didier Drogba, mchezaji mashuhuri wa mpira kutoka Cote d’Ivoire anayechezea timu ya Chelsea ya Uingereza, na kuongoza kwa kufunga magoli mengi zaidi kushinda wachezaji wengine Ulaya hivi sasa, ameteuliwa na Shirika la UM juu ya Miradi ya Maendeleo (UNDP) kuwa Balozi Mfadhili, atakayesaidia kwenye zile juhudi za kuhamasisha umma wa kimataifa kujumuisha mchango wao maridhawa, ili kukamilisha, kwa wakati, yale Malengo ya Maendeleo ya Milenia (MDGs).