1 Disemba 2006
KM Kofi Annan ameripotiwa kushtumu yale mapigano makali yalioshtadi hivi majuzi katika mji wa Malakal, uliopo katika Jimbo la Nile ya Juu, Sudan ya Kusini, uhasama uliozuka kati ya Jeshi la Serekali ya Sudan (SAF) na kundi la waasi la SPLA. Kitendo hiki, alisisitiza KM, kiliharamisha kihakika na kukiuka yale Maafikiano ya Jumla ya Amani.